steve caver/

steve caver/

sTIVE FRIEND

Monday, January 28, 2013

Wasanii wafanya kweli Darlive

  Siku ya jumamosi ya majuzi wasanii wa filamu wote walikutana katika viwanja vya Dar Live katika tamsha la Siku ya Masuper Star Lengo kubwa lilikuwa kujenga urafiki na mashirikika mengine pamoja na kukusanya fedha zitakazo saidia kujenga Ofisi ya hadhi ya shirikisho la Wasanii maarufu kama TAFU chini ya raisi wa shirikisho hilo Simon Mwakifamba.  Katika tamasha hilo pia walimwarika Meya wa Ilala Jery Slaa, huku wasanii wenyewe ndio wakiwa watoa burudani wakubwa katika tamasha hilo

Picha zaidi za wasanii ndani ya ukumbi wa Darlive

















Saturday, January 19, 2013

Mwakifamba ataka wasanii kuwa kitu kimoja

  Shirikisho la wasanii Tanzania 'TAFF' leo limefanya kikao ili kuweza kuangalia ni jinsi gani wanaweza kuendesha shirikisho hilo, kutokana na upungufu wa fedha walizokuwa nazo. Raisi wa shirikisho hilo Simon Mwakifamba, alisema shirikisho hilo halitegemei fedha kutoka Serikalini hivyo ni juhudi zao pekee ndizo zinazoweza kufanikisha kwao. Alisema pia sheria mbalimbali zimekuwa zikiwabana, hivyo huu ni wakati wa wao kuungana na kushikamana ili kuweza kupamba juu ya ufisadi wanaofanyiwa, kwenye tasnia yao kuanzia kwenye sheria ambao inawapa nafasi kubwa Wasambazaji kuwa na haki.
 Dino akiwa na Cloud 112, wakifuatalia kikao
 Dr Cheni akifuatilia kikao kwa umakini
 Wasanii wakifuatitilia kikao

 Nyerere the power akisikiliza mkutano ukiendelea





Ki Utu Uzima yaiva ya Joh Makini


Mwana Fa afungua mwaka na THE FINEST


Saturday, January 12, 2013

Msanii wa filamu apata ajali akatwa mguu

































 Mwigizaji wa filamu wa Rashidi Waziri Matata amepata ajali ya kugongwa na gari leo na kuumia vibaya sana hadi kupelekea kupelekwa katika hospitali ya Taifa Muhimbili na kulazwa katika wodi ya Sewa hadi 18. Taarifa zinadai msanii huyo kwa sasa amekatwa mguu mmja kutokana na ajali hiyo. Wasanii wote wanaombwa kwenda kumuona na kumsaidia msanii mwenzao kwa kile kilichomkuta, kwani kabla hujafa hujaumbika.
Rashidi Waziri Matata akiwa katika moja ya kava la filamu ya Nguvu ya Damu. Nyerere the Power inamtakia nafuu.

Friday, January 11, 2013

Asha baraka asubiri stika za TRA



MKURUGENZI wa bendi ya Twanga Pepeta Asha Baraka, amesitisha utoaji wa filamu  ya Watoto wa mama Ntilie, mpaka zitakapotoka stika za Shirika la Mapato Tanzania ‘TRA’ na kauli ya  Waziri wa Elimu  kuhusu  msaada wa kitabu hicho.
amesema kwa sasa amesitisha kazi zake zote hadi za muziki, hadi stika hizo ambazo zitasiamia kazi za wasanii zitakapotoka hapo mwakani.

Alisema pia yupo kwenye mazungumza na wizara ya Elimu juu ya kusaidia kidogo kuweza kukusambaza filamu hiyo inayotokana na kitabu cha kidato cha tatu na nne.
“Nikitabu ambacho nahitaji kusambaza katika shule za sekondari, ili watoto wajifunze kwa kuangalia” alisema.
Kitabu hicho anatarajia kukisambaza bule katika mashule ya sekondari, na vingine kuviuza kwa bei nafuu kwa watu ambao watakihitaji.


Thursday, January 10, 2013

Mh Temba alizwa

mwanamuziki  wa kizazi kipya Amani Temba ‘Mh Temba’ amesema amerudishwa nyuma sana baada ya kuibiwa vifaa vya gari lake aina ya Verros na mikatamba mbalimbali ya kazi na vitu vingine vilivyokuwemo kwenye gari hilo.

Akizungumza na mwandishi wa safu hii, alivitaja  alisema baadhi ya vifaa walivyoiba ni Power Windor zote, Camera, Dashboard, Cd, mawani na document zingine za kazi zake ikiwemo mikataba ya kazi.
Alisema gari hilo alililaza maeneo ya nyumbani kwake Mbagara ambapo mara nyingi amekuwa akililaza, lakini safari hii alipotaka kwenda kulichukuwa asubuhi alikuta vio vidogo vya nyuma vikiwa vimevyunjwa na kufunguliwa mlango.

“Wamechukuwa haki karatasi ambazo nilikuwa nataka kuzifanyia kazi zangu, mikataba yaani wamenirudisha nyuma sana” alisema.

Baby J na Say Nag kukinukisha Jumapili Billicanas

Wanamuziki wawili kutokea Zanzibar, Baby Ja na Say Nag wanatarajia kuonyeshana umwamba katika Club Billicanas katika juma pili hii, baada ya kuwa katika bifu la maneno kwa muda mrefu. Wasanii kibao wanatarajia kwenda kusindikiza show hiyo, huku kila mmoja akiwa amejipanga na madensa wake kwaajili ya kuonyesha uwezo wake ni bora ya mwenzake.

Wednesday, January 9, 2013

Wanenguaji wa Extra Bongo, watua Twanga

  Bendi ya Twanga Pepeta, imepata wanenguaji wapya ambao wamepania kufanya makubwa kwenye bendi hiyo. Wanenguaji hao wametokea katika bendi ya Extra Bongo, wamesema lengolao kufanya makubwa katika bendi hiyo ya Asha Baraka.  Wanenguaji hao ni  Morine Mishebeduo, Happy wa Danger na Lightness


Safari ya mwisho ya Omari Omari

 Siku ya leo msanii wa muziki wa kizazi kipya ambaye alikuwa akiimba mchiriku (Mnanda) Omari Omari amezikwa katika makabuli ya maeneo ya kwao ya Temeke Mikoroshini. Mwanamuziki huyo mazishi yake yaliudhuliwa na wasanii wengi, lngawa si kama vile watu walivyofikiria. Hata hivyo katika msiba huo, hari ya hewa haikuwa mzuri wakati wa kuzika, baada ya ya vijana kuonyesha kutaka kuzika kama wanavyohitaji wao, na kutokea marumbano kidogo.
 Mwili wa marehemu ulizikwa salama baada ya kufika katika makabuli hayo

 Meneja wa kundi la Tmk na Mkubwa na Wanawe, saidi Fella yeye alijitolea kusimamia shughuli za msiba mpaka zinakwisha.
 Mwanamuziki Juma Kasim Nature akiwa kwenye pozi
 Raisi wa shirikisho la wasanii wa filamu nchini, Saimon Mwakyamba akifurahi akiwa katika msiba.
 Dr Cheni na mzee Yusufu
 Inspecta Haroon

 Dully Syskes
 Ally Jay na mwakilishi wa Bongo Movie Chiki Mchoma.
 Mwanamuziki Dully Syskes, Chege Chigunda na Mwana Fa.




Monday, January 7, 2013

Jk aongoza wasanii kumzika Sajuki

 Raisi wa Tanzania Jakaya Mrisho kikwete jana amekamilisha katika safari ya mwisho ya msanii wa filamu nchini Juma Kilowoko 'Sajuki'katika makabuli ya kisutu jijini Dar es salaam. Katika mazishi hayo yaliyofanyika muda wa saa saba yaliudhuliwa na viongozi mbalimbali, pamoja na wasanii wengine kutoka tasnia mbalimbali kuhakikisha wanakamilisha safari ya mwisho ya msanii huyo ambaye ameteseka kwa muda mrefu kutokana na maradhi ya uvimbe.